Featured

NAMNA YA KUTIBU UGONJWA WA NDUI YA KUKU KWA KUTUMIA DAWA ZA ASILI.

Habari ndugu mfugaji, Karibu UFUGAJIMAKINI ufuge kuku kitaalamu, Ufugajimakini ni Tovuti/Blog ambayo inakupa updates zote za ufugaji wa kuku, kwa hiyo kama ni mara yako ya kwanza kutembelea blog hii basi usisite kuinakili na kuchukua taarifa zake za mawasiliano ili wakati mwingine unapohitaji msaada wa kitaalamu kuhusu ufugaji usiteseke.
Leo ninakuletea Makala hii ya jinsi ya kutiu kuku wako ugonjwa wa ndui kwa kutumia dawa za asili, ugonjwa wa ndui ni ugonjwa unaoenezwa kwa virusi.

DALILI ZA UGONJWA WA NDUI.
·         Uonjwa wa ndui utaona kuku wako wamepata mapele kwenye kichwa yenye rangi ya kahawia, mapele hayo yanaweza kuziba mpaka macho kufanya kuku wako wasione kabisa na kusababisha kuku wako wakashindwa kula hivyo wakadhoofika kabisa na hatimaye kufa. Ugonjwa huu huwapata kuku wa rika zote lakini huathiri sana vifaranga.

Mara nyingi magonjwa ya virusi ni magonjwa ambayo hayana tiba lakini yana kinga. Wachanje kuku wako hasa vifarnga wanapokua wamefikia umri wa siku 56 yani wiki nane(8),  na kama usipowachanja kuku wako na kwa bahati mbaya ugonjwa huu ukaingia bandani kwako basi la kufanya ni hili hapa..
NAMNA YA KUTIBU UGONJWA WA NDUI.
Njia hii nimeshaitumia mara kadhaa pale ugonjwa ulipowapata kuku wangu na ikanipa matokeo chanya kwa asilimia 95%.
Kwana kabisa nunua OTC 20% pamoja na vitamin, wachanganyie kuku wako kwenye maji ili kuwaepusha na magonjwa nyemelezi kwa sababu wanpokua wanashambuliwa na ugonjwa wa ndui ugonjwa wa ndui una sifa ya kupunguza sana kinga ya mwili, kinga ya mwili kwa kuku wako inashuka sana hivyo inakua rahihisi kwa kuku wako kuambukizwa magonjwa mengine, kwa hiyo unapokua unawapatia OTC 20% pamoja na VITAMIN inawasaidia kuboost kinga ya mwili..
Sasa uatafanyaje ili kutibu ugonjwa wa ndui? Kwanza kabisa tafuta mafuta ya ng’ombe yanapatikana masokoni hasa masoko makubwa makubwa unaweza ukanunua maziwa freshi ambayo hayajawekewa maji ukayagandisha alafu ile samli ya juu ukaichukua kama mafuta ya ng’ombe.

Unayafanyaje sasa hayo mafuta ya ngo’mbe, Mafuta hayo unawapakaa kuku wako maeneo ambayo yana hayo madonda. Unapaka mara mbili kwa siku asubuhi na jioni ndani ya siku mbili. Baadae yale madonda yanakua yamelainila na unaweza kuyabandua bila shida yoyota na kuku wako wanakua vizuri na wanakua wamepona.
kama kuna njia nyingine unayoitumia kutibu ugonjwa huu basi usisite kushare na wengine kwa kucoment hapo chini. Ahsante

Subscribe to this Blog via Email :

19 comments

Write comments
sajo
AUTHOR
February 13, 2020 at 9:33 AM delete

asante kwa somo zuri, Kadharika unaweza tumia pia mafuta ya kondoo una pakaa kama ulivyo elekeza. itakupatia majibu chanya

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
March 24, 2020 at 8:42 PM delete

Asate kwa somo njia nyingine in kuwapaka spirit kwenye uvimbe hii inaponesha haraka

Reply
avatar
June 3, 2020 at 7:26 PM delete

yote ni mazuri sana kuna dawa ya asili ya katani unaitwangwa unaipaka kwenye vidonda . magonjwa mengi ya kuku natumia dawa za asili nitafute nikuunge ktk group yetu ya fuga kwa faida no,0755290806

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
August 12, 2020 at 5:50 PM delete

Kuku wangu wangu kama wawili au watatu wanakama vidonda vigumu kwenye sikio kwachini ,ila awaonyeshi kuumwa wanachangamka vizuri nakutaga wanataga sielewi sasa iyo imetokana nanini?
Msaada apo

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
August 14, 2020 at 7:34 AM delete

dawa nyingine ya ndui ni Mtakalang'onyo au Euphorbia, ipo youtube search youtube Tiba za asili za kuku Noah kyando Tv imeelezwa vizur kabisa

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
October 12, 2020 at 11:20 AM delete

Nimeurahi kujua hilo asante mtaalam

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
March 4, 2021 at 6:48 PM delete

Mm nilijaribu kw kuyabandua mapele na kisha kuwapaka ppf ilosagwa pia sio mbaya

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
July 22, 2021 at 9:19 PM delete

Nimejifinza kitu, nashukuru

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
August 10, 2021 at 12:38 PM delete

Njianjia nyingine ya kutibu ndui ya kuku, chukua maji safii yachemshe kias cha uvuguvugu, maji hayo yachanganye na chumvi kias, safisha kile kidonda kwa kukisugua, mwisho chukua aloevera kata kipande mdondoshee ule ute wa njanonjano unaotoka kwe jani la alovera.. fanya hivyo kwa siku mbili kukuwako atapona vzr

Reply
avatar
Unknown
AUTHOR
September 22, 2021 at 9:05 AM delete

Asante kwa makala hii nzuri na ya kuelimisha nimejifunza kitu hapo.

Reply
avatar
Anonymous
AUTHOR
September 10, 2023 at 3:27 PM delete

Na vipi kuhusu jicho kuvimba na kufunga kutoona kabisa

Reply
avatar