
UTANGULIZI
Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na una muda wa kuwahudumia wanyama waha, ufugaji wao si rahisi kama
vile ukifuga paka au mbwa, sungura wanahitaji uangalizi na hassa kwenye
usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira
mabaya na machafu
MABANDA
Kna aina mbili za mabanda ya kufugia kwanza ni yale ya kuwafungia ndani
muda wote bila kutoka nje na ya pili ni ile ya pili ni nusu nusu yaani
wanakuwa na mabanda na wanaweza kutoka nje kwenye ua maalum, katika aina
zote mbili ni muhimu kuhakikisha hakuna upenyo wa kuruhusu panya kupita
kwa sababu huwa wanakula watoto wa sungura.
UFUGAJI WA NDANI
1 - Usitumie banda la kioo (aquarium) kwa sababu halina hewa ya kutosha na ni vigumu kusafisha
2 - Sakafu ya nyavu za waya ni nzuri zaidi ila hakikisha hakuna sehemu
zenye ncha kali inayoweza kuwaumiza sungura, kwani wakumia ni mpaka
wapone wenyewe au umchinje kwa sababu ukitumia dawa za antibiotic
sungura hana uwezo wa kuzimeng'enya na kuisha mwilini mwake, siku
ukimchinja atabakia na dawa na hata ukinusa nyama yake utahisi harufu ya
dawa
3 - Ukubwa wa banda usipungue mita 4 * 2 kwa kila sungura mmoja, likiwa kubwa zaidi ni vizuri
4 - Chini kuwekewe matandazio kama nyasi kavu au maranda ya mbao,
lakini maranda yatokanbayo na miti yenye mafuta kama mi-pine na
mikaratusi hayafai, wawekee kipande cha blanket au taulo la zamani kwa
ajili ya kulalia na kujifungulia hasa kwa wazazi
5 - Ni muhimu kuwawekea sehemu ya kujificha mara wanapohisi hatari, unaweza kutumia mbao, box gumu au plastiki
UFUGAJI WA NJE
1 - Sehemu yote izungushiwe wavu wa kuku kuzuia panya kuingia na wanyama wengine kama paka, mbwa, mwewe nk
2 - Upande mmoja uwe na mabanda, sehemu ya chakula na maji pamoja na kivuli kwa ajili ya sungura kupumzika
3 - Futi moja chini ya udongo kuwe na zege kuzuia sungura kuchimba na kwenda mbali
4 - Eneo la wazi liwe huru na hatari zote za sumu kama dawa za kuulia
wadudu au mbolea, pia majani yaliyoota yasiwe ni yale yenye sumu (waone
wataalamu wakushauri au ng'oa yote)
MAJI
Tumia mabakuli ya kigae, plastiki au jengea kwa saruji, maji yabadilishwe kila siku na vyombo visafishwe kila siku
CHAKULA
Wapewe majani, mabaki ya mboga za jikoni baada ya kuchambuliwa, pia
unaweza kuwawekea pumba au chakula cha kuku (growers mash) kwenye vyombo
maalum kama chakula chenye virutubisho (concentrates)
USAFI
Kila siku jaribu kuondoa uchafu kama vyakula vilivyo mwagika, na kinyesi
kilichoganda kwenya matandazio, fagia na kubadili matandazio angalau
mara moja kwa wiki, manyoya ya sungura mzazi yasiondolewe hii huonyesha
kwamba anakaribia kujifungua watoto
MENO
Wakati mwingine meno
ya mbele hukua sana na kumsababishia usumbufu wakati wa kula, waone
wataalam ukiona ni marefu zaidi na yanahitaji kupunguzwa, dalili kuu ni
sungura kushindwa kula kwa zaidi ya masaa 12
MIGUU
Miguu ya
sungura si kama ya wanyama wengine, nyayo zake zimefunikwa kwa manyoya,
angalia ukiona yananyonyoka kuna tatizo chunguza, kucha zake nazi
huhitaji kupunguzwa zikikua sana
UBEBAJI
Usimbebe kwa kutumia masiki yake huwa wanaumia sana, shika ngozi nyuma ya shingo kama paka ukitaka kumbeba
DAWA
Wapewe dawa ya minyoo kama piperazine kila baada ya miezi mitatu, dawa
za wadudu kama akheri powdeer zinyunyuziwe kwenya mabanda yao kuzuia
viroboto, usiwape dawa nyingine bila ushauri wa kitaalamu, antibiotics
ndio usijaribu kabisa kama nilivyosema mwanzo
Baada ya kujua jinsi ya kufuga Sungura kuna watu wanasema ,sungura
hawawezi kuliwa? lakini mbona watu wanafanya biashara ya kuuza sungura
wa nyama.
wewe unamawazo gani juu ya hii, inalipa?
wasiliana nami..
0759860370