Featured

UFUGAJI WA FUNZA KIBIASHARA NA JINSI YA KUTENGENEZA FUNZA

funza ni nini? 
Funza hawa ni moja tu kati ya hatua za ukuaji za wadudu walukao, watu wengi hufikili hao funza hubaki kuwa funza mpaka mwisho jambo ambalo si la kweli hawa funza ni larval stage ya ukuaji wa wadudu ambapo wadudu hao wapepelukao hutua na kutaga mayai yao.


Wengine wanachukulia hawa wadudu ni uchafu na kinyaa ila FUNZA ni wadudu wenye PROTINI nyingi ambayo INAHITAJIKA sana kwa UKUAJI wa KUKU,SAMAKI,Nguruwe na mifugo mingine.

Utengenezaji wa Funza ktk kulisha mifugo hupunguza sana gharama za Chakula.

Zipo njia nyingi za Kutengeneza FUNZA.Ila NJIA RAHISI ni;Chukua Kinyesi cha Kuku/ng'ombe jaza kwenye dumu lililokatwa kisha weka pumba za mahindi kwa juu halafu nyunyuzia maji kidogo ili kuwavutia NZI waweze kutaga mayai hapo.Endelea kunyunyizia maji kwa siku 2 zaidi kisha acha.SIKU YA 4 FUNZA WATAANZA KUTOKEA,WAKUSANYE,WAOSHE NA KISHA WAPE KUKU WALE WAFAIDI.

Katika Nchi za wenzetu kuna Viwanda kabisa vya Kutengeneza FUNZA ambao hukaushwa na kuuzwa kwa nchi zingine.

Hii inaweza ikawa FURSA PIA hata Hapa Kwetu TANZANIA.Maana ni Rahisi na Soko lake ni Kubwa SANA.Na Ni kitendo cha Wiki Moja TU,unaanza Kula FAIDA za KUTENGENEZA FUNZA.

Subscribe to this Blog via Email :