Featured

KITABU CHA UFUGAJI BORA WA KUKU: UTANGULIZI

UTANGULIZI



Tanzania ni nchi ambayo watu wake ni wafugaji hasa kuku wa kienyeji, ufugaji huu hufanywa hasa na wafugaji wadogo wadogo wahishio maeneo ya vijijini. Ufugaji wa kuku wa kisasa ufanywa hasa na wafugaji wahishio mijini, lakini mahitaji ya Watanzania bado ni makubwa kulingana na idadi (yaani ufugaji wa kuku mjini na vijijinji) na ukilinganisha na ongezeko la watu katika nchi. Vile vile mazao yanayopatikana ni kidogo sana na hafifu.

Kuku wa kienyeji kwa wastani anataga mayai 40 hadi 60 kwa mwaka badala ya mayai 80 hadi 100 kwa mwaka kama atatunzwa vizuri. Hali kadhalika wastani wa uzito wa kuku mmoja ni wa chini sana (kilo 0.75 hadi 1.0) katika umri wa zaidi ya mwaka mmoja: Iwapo atatunzwa kwa kufuata kanuni za utugaji bora ana uwezo wa kufikia uzito wa kilo 1.0 hadi 1.5.

Kuku wa kisasa ana uwezo wa kutaga mayai zaidi ya 250 kwa mwaka na kuwa na uzito wa kilo 1.5 hadi 2 katika umri wa miezi miwili (wiki nane). Uzalishaji mdogo wa kuku hawa unatokana na kutokuwepo kwa utaalamu wa kutosha wa utunzaji wa kuku wa kienyeji. Vile vile matunzo ya kuku wa kisasa hayajafikia kiwango kinachotakiwa.

Ili mfugaji aweze kujipatia mazao mengi na bora ni muhimu azingatie kanuni za ufugaji bora wa kuku. Kanuni hizo ni pamoja na ujenzi wa mabanda bora ya kuku na vifaa vinavyohitajika katika mabanda hayo, uchaguzi wa njia sahihi za ufugaji, jinsi ya kutunza kuku wa kienyeji na wa kisasa. Kanuni zingine ni pamoja na namna ya kutengeneza chakula bora cha kuku, jinsi ya kuzuia magonjwa, utafutaji wa masoko na utayarishaji wa mazao kabla ya kuuza. Maelezo yaliyomo katika kitabu hiki yakizingatiwa yatawawezesha Watanzania kujipatia nyama na mayai mengi ambayo yataongeza ubora wa afya zao na kuinua hali za maisha ya Watanzania kwa kuuza mazao ya ziada.

Ni matumaini yangu kuwa kitabu hiki kitawasaidiwa watu wengi ambao wamekuwa na changamoto ya ufugaji wa kuku kwa muda mrefu. Kama kuna lolote basi msisite kuwasiliana nami kupitia utaratibu wowote kati ya hizo zilizoelekezwa mwishoni mwa kitabu.

GHARAMA ZA KITABU HIKI NI TSH 6000 > NAKALA LAINI (0752438521)

Subscribe to this Blog via Email :

1 comments:

Write comments