Featured

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA ILI KUFANIKISHA CHANJO BORA

Chanjo mbalimbali za kukinga magonjwa zina utaratibu wake kitaalamu, kama namna ya utunzaji na 
namna kuwapa kuku. Zifuatazo ni dondoo muhimu za kufahamu ili chanjo yako ifanikiwe;
1. Ukihifadhi chanjo yako hovyo hovyo bila kufwata maelekezo ya kitaalamu, chanjo hiyo inakua Sumu 
badala ya kuwa kinga na tiba. Chanjo iliyohifadhiwa vibaya haiwezi kufanikisha matibabu. Chupa za chanjo 
huwa zinakuwa na lebo au karatasi yenye maelekezo ya jinsi ya kutumia pamoja na tarehe ya mwisho ya 
matumizi (Expire date). Usipochanja kuku wako vizuri, ugonjwa unaweza kuenea zaidi.
2. Vifaranga vilivyoanguliwa huweza kuwa na magonjwa mbalimbali yaliyotoka kwa Mama kuku, kupitia 
yai. Kwa hiyo kuwachanja kuku walio na umri chini ya siku kumi (10) ni muhimu sana, kwa sababu itazuia 
magonjwa ambukizi kwa vifaranga kadri wanavyokua.
3. Kila chanjo imetengenezwa kwa kuwekwa mahali sahihi kwenye mwili wa kuku, kuna baadhi huwekwa 
kwenye macho, baadhi kwenye maji na baadhi huchomwa kwa sindano kwenye mabawa. Kwa hiyo 
usibadilishe matumizi ya chanjo.
4. Usiwape chanjo kuku Waliokwisha kuugua [Isipokua kama kuna mlipuko wa ugonjwa wa 
Laryngotracheitis au Fowl pox]
5. Hifadhi chanjo mahali salama pasipokua na joto & mwanga wa jua wa moja kwa moja.
6. Chanjo zilizo nyingi ni viumbe hai visivyoonekana kwa macho (Living micro-organisms) au chembe 
chembe zinazotengeneza magonjwa (disease-producing agents), Kwa hiyo hifadhi chanjo zako kwa 
Uangalifu.
7. Kama unatumia maji ya kunywa kuku kama njia ya kuwapa chanjo, hakikisha Unatumia maji yasiyokua 
na chumvi na Chlorine, kwa sababu chembechembe au viumbe waliopo kwenye chanjo huharibiwa na hizo 
kemikali.
8. Baada ya kutoa chanjo hakikisha unachoma au unavitibu (Kuosha na Kemikali inayoua vimelea vya 
magonjwa, Disinfect) vifaa vyote ulivyotumia wakati wa kutoa chanjo. Ukifanya hivi utazuia kueneza 
magonjwa kwa kuku wazima wasiokua magonjwa.


Subscribe to this Blog via Email :