Featured

KUCHAGUA MAYAI KWA AJILI YA KUATAMIA

KUCHAGUA MAYAI KWA AJILI YA  KUATAMIA
👍Tumia mayai yaliyotagwa si zaidi ya wiki mbili zilizopita.

👍Angua vifaranga kwa kutumia mama kuku, au kuku wengine wanaoatamia, au bata au mashine ya 
kutotoreshea (incubator).

👍  Kwa kuku na bata hakikisha unawapa idadi ya mayai kulingana na ukubwa wa maumbile yao, yaani 
lazima mayai yatoshe chini ya matumbo yao wakati wa kuatamia.

👍Baada ya kuangua mayai safisha maeneo ya kutagia pamoja na kutupa maganda ya mayai 
yaliyoanguliwa.

👍Kama unatumia mashine ya kuangulia mayai, hakikisha unageuza mayai angalau kwa siku mara 3, 
isipokua siku tatu za mwisho kuelekea kuangua vifaranga (Siku ya 1 hadi 18: Geuza mayai, Siku ya 19 
hadi 21: Usigeuze mayai)

Subscribe to this Blog via Email :