Featured

MAMBO 7 YA KUZINGATIA KATIKA ULEAJI WA VIFARANGA

UTANGULIZI
Imekuwa changamoto sana kwa wafugaji wengi. Na mara nyingi kwa wale wanaoanza ufugaji, ufikia hatua hadi kukata tamaa. 

Wakina mama wamekuwa waleaji wazuri sana wa vifaranga. Kwa sababu, wamejifunza tabia ya kuangalia hali ya mtoto wake kila saa. Na vifaranga wanahitaji uangalizi wa hali ya juu sana, ile week ya kwanza.

Leo, natamani ujifunze vitu 7 vya msingi sana katika uleaji wa vifaranga wako.

1. Hakikisha unaweka matandiko safi na salama bandani, urefu wa 5cm. 

2. Hakikisha kuna joto 28’C - 32’C bandani. Kadri vifaranga wanavyokuwa, joto lipunguzwe bandani.

3. Hakikisha kuna hewa safi bandani. Ukiingia bandani hakikisha hamna hewa yenye harufu mbaya

4. Hakikisha kuna mzunguko mzuri wa hewa bandani.

5. Vifaranga wapewe maji safi Na Salama. Vifaranga wanahitajika kunywa maji mengi sana

6. Chakula chenye lishe bora kwa vifaranga.

7. Wiki ya kwanza, hakikisha kuna mwanga muda wote bandani.Vifaranga waweze kula 

Imeandakiwa na #ufugajimakini

Subscribe to this Blog via Email :