Featured

UFUGAJI NA UANGALIZI WA KWARE 🐥

*UFUGAJI WA KWARE :*


Sehemu ya Kwanza

Utayarishaji wa banda, Utagaji na uatamiaji mayai, utunzaji vifaranga, uleaji wa vifaranga magonjwa, tiba na kinga.

🔹UTANGULIZI:

Kware ni ndege mdogo mwenye asili ya toka huko Japan. Wakiwa mwituni kware ni ndege wanaohama hama na kuishi mashambani. Rangi ya kware huyu wa mjapan ni yenye madoadoa ya kahawia meupe na meusi yanayoanzia kichwani mwake na hadi mkiani tumboni akiwa na rangi ya kahawia hafi fu. kware pia wanapatikana katika rangi tofauti kama nyeupe tupu, au nyeupe na nyeusi, Kware mkubwa anaweza kuwa na uzito upatao wa gramu 150.

🔹BANDA:

Banda liwe na sifa kama banda la kuku. Kwa kuanza unaweza ukawa na banda la ukubwa wa 1.5m x 1.5m, pia lazima uzingatie usalama
wa vifaranga dhidi ya panya, paka au vicheche. Unatakiwa kuweka ‘magazeti au makasha’ chini kwenye sakafu yatakayosaidia kuondoa hali ya unyevunyevu na pia inakuwa rahisi kulifanyia usafi.

🔹UTAGAJI MAYAI

Wiki ya sita kuelekea ya saba kware wataanza kutaga mayai kila siku. Kwa wastani kware mmoja hutaga mayai 24.

Kware dume humpanda jike kwa muda kidogo, Hapo jike anakuwa tayari kutaga na hutaga mayai 290 hadi 310 kwa mwaka (hii hulingana na lishe nzuri atakayopatiwa).

Mayai ya kware huatamiwa kwa siku 16 na huanza kuanguliwa vifaranga kwa muda wa siku 2, kuanzia siku ya 16 na hadi 18.Njia bora ya kutotolesha mayai ya kware ni kwa kutumia incubator ambapo mayai huatamiwa kwa wingi ndani ya siku 18.


UTUNZAJI WA VIFARANGA

🔹JUMA LA KWANZA

 Vifaranga wapatiwe chakula “Broiler starter” na maji masafi ya kutosha. Siku ya 1 wawekee ‘GLUCOSE’ kwenye maji, Packet moja kwa lita 6 za maji, na siku ya pili hadi ya tano wape vitamini kama vitalyte kwenye maji, siku ya sita wape vitamini pekee kama Stressvita/Farmvita na siku ya saba wapatie chanjo ya Newcastle.

USAFI: Katika juma hili la kwanza chakula kitawekwa chini na tunashauri kuhakikisha vifaranga hawatelezi na kuathiri miguu.

🔺ZINGATIA: Weka goroli au mawe kwenye manywesheo (drinkers) zako ili kuzuia vifaranga wasizame ndani ya (drinkers) maji na kufa.

🔹JUMA LA PILI: 

Vifaranga wataendelea kupewa chakula Broiler starter na maji safi. Wataendelea kuhitaji ‘mwanga’ wa kutosha muda wote na joto la wastani.

🔹JUMA LA TATU

Uhitaji wa joto utapungua, ila ni kipindi ambacho wanakula chakula zaidi kwa ajili ya kukua. Ni vizuri waendelee kupata taa ili kupata mwangaza utakaowawezesha kula mchana na usiku.

🔹SIKU 21 NA KUENDELEA

KWARE wako hawatahitaji joto tena wawekee taa tu za chemli au energy server kipindi cha usiku, wape chakula na maji ya kutosha zaidi kwa ajili ya kukua.


⚠️ MAGONJWA:

KWARE ni ndege wenye kinga kubwa na ni vigumu sana kushambuliwa na magonjwa kama kuku na mara wanapougua ni rahisi sana kutibika. Magonjwa yanayoweza kuwapata kware ni typhoid, mafua na E.Coli.

🔹TIBA KWA KUTUMIA DAWA ZA DUKANI:

Amprolium kwa ugonjwa wa kuharisha damu/ugoro (Coccidiosis), Fluban, Colirid au Doxycol kutibu mafua (Coryza) na Esb3, au Trimazine, Typhoprim, Ancoban hutumika kwa homa ya matumbo (Typhoid).

🔹TIBA MBADALA

Waweza kuwatibu vifaranga au kware wako kwa kutumia tiba mbadala ambayo pia ni rahisi, gharama nafuu na bora zaidi kuliko kutumia madawa yaliyochanganywa na kemikali na yenye gharama. Vifuatavyo ni vitu vya asili vinavyotumika kutibu magonjwa mbali mbali ya kware na yanayopatikana kwa wingi katika maeneo ya mfugaji. Madawa haya hutumika kwa kiwango cha wastani na hayana kipimo maalum kwani hata ukiyazidisha hayana madhara.

🔹MAJANI YA MWAROBAINI

Madawa haya hutumika kutibu kuharisha damu pamoja na mafua kwa vifaranga vya kware Chukua kiasi kidogo cha mwarubaini kisha twanga vizuri kupata maji maji. Kamua maji yale, kisha weka katika maji uliyoandaa kuwanywesha vifaranga wako. Kata vipande
vidogovidogo vya aloe vera (jani moja laweza kutosha) na tia katika maji yaliyochanganywa na mwarobaini, kisha wapatie vifaranga wanywe (Aloe Vera) itaendelea kujikamua yenyewe ikiwa ndani ya maji huku vifaranga wakiendele kunywa).

🔹KITUNGUU SWAUMU:

Hii hutumika kukinga na kutibu vifaranga vya Kware wanaosumbuliwa na kuharisha damu. Unachukua kitunguu swaumu na kuondoa maganda ya nje kisha kusafi sha na kukata vipande vidogo sana, na kuwawekea kama chakula. Vifaranga wanapenda sana vitunguu hivyo na watakula kwa kasi kama chakula lakini ni tiba tayari. Unaweza kuwapatia kila siku hadi watakapopona.

🔹MAZIWA:

Maziwa yanayotokana na ng’ombe pia hutumika kutibu ugonjwa wa kuhara pamoja na kuwapa nguvu kware waliolegea. Mnyweshe maziwa hayo kware anayeumwa bila kuyachemsha na umnyweshe maziwa ya kutosha kiasi cha kushiba. Unamnywesha mara tatu kwa siku. Hakikisha maziwa unayotumia yanatoka kwa ng’ombe wanaotibiwa kila mara.

⚠️ ANGALIZO:

Siyo lazima kwale waugue ndipo uwapatie tiba hizi. Hakikisha unawapa tiba kabla hata hawajaugua hivyo utawakinga na magonjwa hayo. Waweza kuchanganya madawa hayo yote kwa wakati mmoja kwani hayana madhara.

Endapo madawa ya asili hayapatikani katika eneo la mfugaji basi waweza kuwatibu kwale kwa madawa yafuatayo ambapo vipimo huelezwa moja kwa moja kwa maandishi katika madawa hayo au kuelezwa na muuzaji pale utakaponunulia

🔺CHANJO

Kware wapatiwe chanjo ya “kideri/mdondo” kwa dawa inayoitwa ‘Newcastle’ lasota au T2. Siku ya 7. Chanzo cha maambukizi ni maji na chakula kilichochafuliwa na kinyesi na pia husababishwa na virusi kwa njia ya hewa.

Wapewe chanjo ya “gumboro”. inapofi ka Siku ya 14.

Siku ya 21 lazima warudie chanjo ya “Newcastle” na kila baada ya miezi 3 na hakikisha unarudia chanjo ya Newcastle.

Subscribe to this Blog via Email :